Swali: Ni ipi hukumu ya ambaye amehifadhi sehemu katika Qur-aan kwa ajili ya selibasi ya masomo kisha baada ya matokeo ya mtihani hafuatilizi kile alichohifadhi na akaw amekisahau. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Naona kuwa uhalisia wa mambo ni kwamba mtu huyu amekhasirika na ameenda kinyume maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Ipatilizeni Qur-aan. Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake inaponyoka haraka kuliko ngamia kwenye kamba yake.”
Nasema midhali Allaah amekuneemesha kuhifadhi kile kilichokusahilikia katika Qur-aan, basi akipatilize na airudirudi Qur-aan. Kwani:
“Hakika mbora wenu yule aliyejifunza Qur-aan na akawafunza wengine.”
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (40) http://binothaimeen.net/content/903
- Imechapishwa: 22/08/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)