Swali: Nini hukumu ya kuongeza maneno:
وبركاته
“… na baraka Zake.”
katika salamu ya kumaliza swalah?
Jibu: Dhaifu, yanapingana na yaliyo Swahiyh. Masimulizi hayo yanahitaji kuangaliwa vyema. Yana udhaifu. Kilicho Swahiyh na kilichohifadhiwa ni kuishilia kusema:
ورحمة الله
”… na rehema za Allaah.”
kama ilivyo katika Hadiyth ya Ibn Mas’uud, Samurah bin Jundub na Sa’ad bin Abiy Waqqaas. Ingawa al-Haakim (Rahimahu Allaah) ameisahihisha, lakini bado kuna shaka juu ya usahihi wake kwa sababu inatokana na masimulizi ya ´Alqamah kwa kunukuu kwa njia isiyokuwa wazi na hakusikia moja kwa moja kutoka kwa baba yake. Kwa ajili hiyo Ibn Ma’iyn na wanazuoni wengine wamesema kuwa ´Alqamah hakuisikia kutoka kwa baba yake, ingawa baadhi ya wanazuoni wamesema kuwa amesikia baadhi ya mambo kutoka kwake. Hata hivyo baadhi ya masimulizi ndani ya ”as-Swahiyh” ya Muslim zinataja kwamba ´Alqamah alisikia kutoka kwa baba yake.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24863/حكم-زيادة-وبركاته-في-التسليم-من-الصلاة
- Imechapishwa: 02/01/2025
Swali: Nini hukumu ya kuongeza maneno:
وبركاته
“… na baraka Zake.”
katika salamu ya kumaliza swalah?
Jibu: Dhaifu, yanapingana na yaliyo Swahiyh. Masimulizi hayo yanahitaji kuangaliwa vyema. Yana udhaifu. Kilicho Swahiyh na kilichohifadhiwa ni kuishilia kusema:
ورحمة الله
”… na rehema za Allaah.”
kama ilivyo katika Hadiyth ya Ibn Mas’uud, Samurah bin Jundub na Sa’ad bin Abiy Waqqaas. Ingawa al-Haakim (Rahimahu Allaah) ameisahihisha, lakini bado kuna shaka juu ya usahihi wake kwa sababu inatokana na masimulizi ya ´Alqamah kwa kunukuu kwa njia isiyokuwa wazi na hakusikia moja kwa moja kutoka kwa baba yake. Kwa ajili hiyo Ibn Ma’iyn na wanazuoni wengine wamesema kuwa ´Alqamah hakuisikia kutoka kwa baba yake, ingawa baadhi ya wanazuoni wamesema kuwa amesikia baadhi ya mambo kutoka kwake. Hata hivyo baadhi ya masimulizi ndani ya ”as-Swahiyh” ya Muslim zinataja kwamba ´Alqamah alisikia kutoka kwa baba yake.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24863/حكم-زيادة-وبركاته-في-التسليم-من-الصلاة
Imechapishwa: 02/01/2025
https://firqatunnajia.com/kuongeza-wa-barakaatuh-katika-salamu-ya-swalah-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)