Swali: Kuongeza:
وبركاته
”… na baraka Zake.”
katika salamu baada ya kumaliza kuswali?
Jibu: Imepokelewa katika baadhi ya mapokezi ambayo baadhi yake yana udhaifu. Maoni yaliyo karibu zaidi na usahihi ni kuishilia:
رحمة الله
“… na rehema za Allaah.”
kama alivyosimulia Samurah ambaye amesema:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema:
السلام عليكم ورحمة الله، السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu, Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
Swali: Nyongeza:
وبركاته
”… na baraka Zake.”
ni dhaifu?
Jibu: Ndio, inapingana na Hadiyth Swahiyh. Salamu ya kumaliza kuswali mtu aseme:
السلام عليكم ورحمة الله
“Amani na rehema za Allaah ziwe juu yenu.”
Lakini mtu anaposalimiana na watu ndio kukamilifu zaidi. Nakusudia mtu anaposalimiana na watu.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23383/حكم-زيادة-وبركاته-في-السلام-من-الصلاة
- Imechapishwa: 07/01/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)