Kunyanyua mikono kuomba du´aa baada ya swalah hakuna msingi

Swali: Je, inajuzu kuomba du´aa kwa kuinua mikono baada ya swalah?

Jibu: Haina asili. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiinua mikono baada ya kutoa salamu. Bali alikuwa akiomba du´aa baina yake na nafsi yake. Hivyo basi watu wasiinue mikono baada ya salamu, si baada ya Dhuhr, ´Aswr, Maghrib, ´Ishaa wala Fajr. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wala Maswahabah wake (Radhiya Allaahu ´anhum) hawakufanya hivyo. Ama mtu kuomba du´aa baina yake na nafsi yake baada ya Dhikr, hilo halina tatizo.

Swali: Vipi ikiwa ni baada ya swalah za Sunnah?

Jibu: Baada ya swalah za Sunnah, akifanya hivyo katika baadhi ya nyakati, hakuna tatizo. Lakini Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwa akiendelea kulifanya jambo hilo kila mara. Kwa hiyo akifanya mara moja na akaacha mara nyingine, ni vizuri, au ikamtokea du´aa fulani ambapo akaamua kuinua mikono na kuomba.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/2451/حكم-رفع-اليدين-بالدعاء-عقب-الصلوات
  • Imechapishwa: 29/03/2026