Kuna haja kwa imamu kuwahimiza maamuma kunyoosha safu kama tayari safu zimenyooka?

Swali: Ikiwa safu zimekwishanyooka – je, inasuniwa imamu kuwaambia:

“Sawazisheni safu zenu na karibianeni”?

Baadhi ya watu huchukulia kama ni Sunnah iliyothibiti, ni mamoja iwe safu imepinda au imenyooka?

Jibu: Imamu anapaswa kuwakumbusha ili wazowee jambo hilo na walitambue. Awe mwenye kuwageukia na kusema:

“Sawazisheni na nyoosheni safu zenu.”

ili wajue umuhimu wa jambo hilo na walizoe.

Swali: Je, imamu awageukie kwa uso wake wakati akisema hivyo?

Jibu: Ndio.

Swali: Ikiwa safu tayari ziko sawa – je, bado ni Sunnah kwake kuwaambia hivo?

Jibu: Haijalishi kitu, aseme hivo ili watu waendelee kulizoea. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa kila akisimama kwa ajili ya swalah alikuwa akiwaambia watu maneno hayo.

Swali: Hivyo ni Sunnah?

Jibu: Ndio.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31147/هل-يسن-للامام-قول-استووا-والصفوف-مستوية
  • Imechapishwa: 07/10/2025