Kujiombea au kumuombea mtu maisha marefu

Swali: Kuomba du´aa ya maisha marefu?

Jibu: Imepokelewa kwamba ´Umar na wengine wamechukizwa na hilo. Hata hivyo itafaa mtu akifunganisha na jumla `.. kwa kumtii Allaah`, `… kwa kumridhisha Allaah`. Wale ambao wameona kuwa inachukiza ni kwa sababu maisha marefu yanaweza kuwa ima na shari na yanaweza kuwa pia na kheri. Ikiwa ni maisha marefu katika mambo ya kheri ni jambo linatakikana:

”Mbora wa watu ni yule ambaye umri wake umerefuka na matendo yake yakawa mema.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24292/حكم-الدعاء-بطول-العمر
  • Imechapishwa: 24/09/2024