Swali: Ni ipi hukumu ya kufuga ndege na kuwaweka kwenye mabanda hawatoki humo huku wakipewa chakula na kinywaji?
Jibu: Hakuna ubaya katika hilo. Ndege katika vizimba pamoja na kuwafanyia wema na kutowapuuza, hakuna tatizo. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba alikuwa akipita kwa mtoto wa Abu Twalhah – ndugu yake Anas kwa mama yake – alikuwa na ndege anayeishika na kucheza nayo, na alikuwa akisema:
”Nini kimemtokea an-Nughayr, ee Abu ´Umayr?”
Kwa hiyo kushika ndege na kuwaweka majumbani ni jambo la zamani. Hakuna ubaya ikiwa ndege wanatunzwa na haki zao hazipuuzwi.
Swali: Kuna wengine ni ndege wakali wanauzwa wanaitwa ndege wa mapambo?
Jibu: Siwajui, kwa vyovyote vile hakuna ubaya ikiwa wamewindwa na hawamdhuru yeyote.
Swali: Ikiwa wanazuiliwa uhuru wao na hatimaye wanakufa ndani ya kizimba, kwa sababu wanahisi kunyimwa uhuru wao na kuruka angani?
Jibu: Hapana, hawafi. Tunajua ndege hadi sasa kwa miaka mingi wako hai.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3380/حكم-اقتناء-الطيور-وحبسها-في-اقفاص
- Imechapishwa: 16/09/2026
Swali: Ni ipi hukumu ya kufuga ndege na kuwaweka kwenye mabanda hawatoki humo huku wakipewa chakula na kinywaji?
Jibu: Hakuna ubaya katika hilo. Ndege katika vizimba pamoja na kuwafanyia wema na kutowapuuza, hakuna tatizo. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba alikuwa akipita kwa mtoto wa Abu Twalhah – ndugu yake Anas kwa mama yake – alikuwa na ndege anayeishika na kucheza nayo, na alikuwa akisema:
”Nini kimemtokea an-Nughayr, ee Abu ´Umayr?”
Kwa hiyo kushika ndege na kuwaweka majumbani ni jambo la zamani. Hakuna ubaya ikiwa ndege wanatunzwa na haki zao hazipuuzwi.
Swali: Kuna wengine ni ndege wakali wanauzwa wanaitwa ndege wa mapambo?
Jibu: Siwajui, kwa vyovyote vile hakuna ubaya ikiwa wamewindwa na hawamdhuru yeyote.
Swali: Ikiwa wanazuiliwa uhuru wao na hatimaye wanakufa ndani ya kizimba, kwa sababu wanahisi kunyimwa uhuru wao na kuruka angani?
Jibu: Hapana, hawafi. Tunajua ndege hadi sasa kwa miaka mingi wako hai.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3380/حكم-اقتناء-الطيور-وحبسها-في-اقفاص
Imechapishwa: 16/09/2026
https://firqatunnajia.com/kufuga-ndege-na-kuwaweka-ndani-ya-banda/