Yule ambaye amejizoweza kusimama usiku ndani ya Ramadhaan basi ahakikishe anaendelea kufanya kuswali kiasi anachoweza. Yule ambaye amejizoweza kufunga basi basi ahakikishe anaendelea kufunga kiasi anachoweza. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu kusimama usiku katika Ramadhaan:
“Yeyote mwenye kusimama katika Ramadhaan kwa imani na kwa matarajio, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
Vivyo hivyo kuhusu swawm za kujitolea ambazo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema juu yake:
“Yule atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia [siku] sita za Shawwaal, basi anakuwa kama amefunga mwaka mzima.”[1]
Masiku sita haya ya Shawwaal ni mamoja yamefungwa mwanzoni mwa Shawwaal, katikati yake au mwishoni mwake, yote yamefungwa kwa kufuatanisha au kwa kuachanisha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kufunga siku sita kila mwezi ni kama amefunga mwaka mzima.”
Ichunge afya yako kwa kufunga. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunga jumatatu na alkhamisi na akaulizwa juu ya hilo ambapo akasema:
“Matendo yanadhihirishwa jumatatu na alkhamisi. Napenda matendo yangu yadhihirishwe ilihali nimefunga.”
[1] al-Bukhaariy na Muslim.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 10
- Imechapishwa: 28/01/2025
Yule ambaye amejizoweza kusimama usiku ndani ya Ramadhaan basi ahakikishe anaendelea kufanya kuswali kiasi anachoweza. Yule ambaye amejizoweza kufunga basi basi ahakikishe anaendelea kufunga kiasi anachoweza. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu kusimama usiku katika Ramadhaan:
“Yeyote mwenye kusimama katika Ramadhaan kwa imani na kwa matarajio, basi atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia.”
Vivyo hivyo kuhusu swawm za kujitolea ambazo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema juu yake:
“Yule atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia [siku] sita za Shawwaal, basi anakuwa kama amefunga mwaka mzima.”[1]
Masiku sita haya ya Shawwaal ni mamoja yamefungwa mwanzoni mwa Shawwaal, katikati yake au mwishoni mwake, yote yamefungwa kwa kufuatanisha au kwa kuachanisha. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kufunga siku sita kila mwezi ni kama amefunga mwaka mzima.”
Ichunge afya yako kwa kufunga. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunga jumatatu na alkhamisi na akaulizwa juu ya hilo ambapo akasema:
“Matendo yanadhihirishwa jumatatu na alkhamisi. Napenda matendo yangu yadhihirishwe ilihali nimefunga.”
[1] al-Bukhaariy na Muslim.
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 10
Imechapishwa: 28/01/2025
https://firqatunnajia.com/kuendelea-kufunga-baada-ya-ramadhaan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)