Kuacha swalah ya mkusanyiko msikitini kwa sababu ya Ruqyah

Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kushughulika na kuwasomea watu Ruqyah na hivyo akaacha swalah ya mkusanyiko msikitini?

Jibu: Hili ni kosa kubwa. Haijuzu kwa chochote kumshughulisha na swalah, sawa ikiwa ni Ruqyah au kitu kingine. Huu sio udhuru kwa kuacha swalah ya mkusanyiko msikitini. Anaweza kurudi na kuendelea kusoma Ruqyah.

Isitoshe, sijui ni Ruqyah sampuli gani hii. Ruqyah leo imekuwa ni biashara. Watu wanatajirika nayo. Imekuwa tena sio kuwafanyia watu wema. Imekuwa watu wanatajirika nayo na wanapetuka kwayo. Wamejiingiza katika mambo haya watu wasiojua Ruqyah. Bali ndani ya Ruqyah kumeingia mpaka mambo ya shirki na watu kuyaomba msaada majini kwa madai ya kwamba ni majini Waislamu na inafaa kwetu kuwaomba msaada. Watu hawa wameingiza utata kwa watu kwa kutumia jina la Ruqyah. Ruqyah leo imekuwa inatumiwa vibaya.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (75) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-11-05.mp3
  • Imechapishwa: 22/08/2020