Kuhusu Qutbiyyah, ni watu wanaosoma vitabu vya Sayyid Qutwub na kumfuata kwa kila alichokisema na kukiamini. Wanamuadhimisha kwa kiwango cha kwamba, wanaonelea kuwa yote anayoyasema ni sawa na ni sahihi hata kama atakuwa anaenda kinyume na dalili na mfumo wa Salaf. Kinachoweka wazi hilo ni uasi wao wa kimatamshi na propaganda zao dhidi ya Shaykh Rabiy’ bin Haadiy al-Madkhaliy tangu alipoanza kuraddi makosa ya Sayyid Qutwub katika ´Aqiydah. Wamefanya akaonekana kama mdhulumaji na mkandamizaji. Uadilifu haukuwafanya kamwe kuweza kurejea katika namba za kurasa ambazo Shaykh Rabiy’ alizotaja katika kitabu chake; kama matusi yake kwa Mtume wa Allaah Muusa (‘alayhis-Salaam), kufasiri kwake kimakosa uongozi wa ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhu) na kuonelea kuwa ilikuwa ni utupu, matusi yake kwa Maswahabah wengine, ujinga wake juu ya Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah, mfumo wa Ash’ariy juu ya Sifa anazoziwekea taawili, mambo ya ´Aqiydah ambayo anayadharau na mengine mengi.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Mawrid al-´Adhb az-Zulaal, uk. 221
  • Imechapishwa: 23/04/2015