Swali: Kuna baadhi ya watu wanaishia tu katika Khutbah ya pili kuleta “al-Hamdu, Shahaadah mbili na ibara zilizopokelewa kama “fa inna aswdaqah al-Hadiyth Kitaab-ul-Laah, kumswalia Mtume (´alayhis-Salaam), kuwatakia radhi Makhaliyfah na Maswahabah wengine na Du´aa bila ya kuzungumzia kitu katika Khutbah ya pili. Ni yapi maoni kwa hilo?

Jibu: Lililo la wajibu ni kuleta mawaidha kwa kuwa Khutbah ya pili ni kama ya kwanza. Hivyo ni lazima kuleta mawadha. Baada ya hapo ndipo ataleta mambo haya. Ama kuishia tu kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mpaka mwisho, ni lazima baada ya kusema “Amma ba´d”, awakumbushe na kuwawaidhisha watu kwa kusoma Aayaat au Ahaadiyth ambazo atawasomea na awakumbushe kwazo. Halafu baada ya hapo ndio akamilishe. Khutbah hii ni kama ile ya kwanza.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=14485
  • Imechapishwa: 03/12/2014