Swali: Akiniomba mzushi kwenda katika msikiti wao kuwatolea mawaidha na Khutbah, nende au nikatae?
Jibu: Usikatae endapo Ahl-ul-Bid´ah watakuomba kwenda katika msikiti wao kwa ajili ya kuwatolea Khutbah, mawaidha au semina au muhadara. Lakini unalazimika kuzungumzia zile Bid´ah walizonazo. Zitahadharishe na bainisha madhara yake kwa dalili za Qur-aan na Hadiyth. Pengine Allaah kupitia kalima, mawaidha au Khutbah akamwongoza wa kumwongoza. Hivyo ukalipwa thawabu kwa jambo hilo.
- Muhusika: ´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=tsr2zBvUy0Y
- Imechapishwa: 16/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)