Swali: Siwaak wakati wa Khutbah ya ijumaa?

Jibu: Haijuzu wakati wa Khutbah. Anyamaze na aache kutikisika. Asitumie Siwaak wala kitu kingine. Anyamaze na kumsikiliza Khatwiyb. Asijishughulishe na Siwaak wala kitu kingine.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22647/حكم-استعمال-السواك-اثناء-خطبة-الجمعة
  • Imechapishwa: 14/07/2023