Swali: Ni ipi hukumu ya kumsalimia muislamu kwa kusema:
السلام على من اتبع الهدى
“Amani iwe juu ya yule mwenye kufuata uongofu?”
Muislamu asalimie vipi waislamu waliokusanyika sehemu moja na makafiri?
Jibu: Haijuzu kwa mtu kumsalimia muislamu mwenzie kwa kusema ´as-Salaam ´alaa manit-Taba´ al-Hudaa”. Kwa kuwa formula hii aliisema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi alipowaandikia wasiokuwa waislamu. Muislamu mwenzie mwambie:
السلام عليكم
“Amani iwe juu yenu.”
Ama kusema ´as-Salaam ´alaa manit-Taba´ al-Hudaa” hiyo inapelekea mtu kufahamu kuwa ndugu yako huyu sio katika wanaofuata uongofu.
Ikiwa waislamu wamekusanyika sehemu moja na manaswara, basi awasalimie salamu ya kawaida kwa kusema:
السلام عليكم
“Amani iwe juu yenu”
na huku akiwakusudia wale waislamu.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/35)
- Imechapishwa: 06/06/2017
Swali: Ni ipi hukumu ya kumsalimia muislamu kwa kusema:
السلام على من اتبع الهدى
“Amani iwe juu ya yule mwenye kufuata uongofu?”
Muislamu asalimie vipi waislamu waliokusanyika sehemu moja na makafiri?
Jibu: Haijuzu kwa mtu kumsalimia muislamu mwenzie kwa kusema ´as-Salaam ´alaa manit-Taba´ al-Hudaa”. Kwa kuwa formula hii aliisema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi alipowaandikia wasiokuwa waislamu. Muislamu mwenzie mwambie:
السلام عليكم
“Amani iwe juu yenu.”
Ama kusema ´as-Salaam ´alaa manit-Taba´ al-Hudaa” hiyo inapelekea mtu kufahamu kuwa ndugu yako huyu sio katika wanaofuata uongofu.
Ikiwa waislamu wamekusanyika sehemu moja na manaswara, basi awasalimie salamu ya kawaida kwa kusema:
السلام عليكم
“Amani iwe juu yenu”
na huku akiwakusudia wale waislamu.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/35)
Imechapishwa: 06/06/2017
https://firqatunnajia.com/inafaa-kumsalimia-muislamu-as-salaam-alaa-manit-taba-al-hudaa/