Swali: Je, mtu akate swalah yake akiswali karibu na mtu aliyekula kitunguu saumu na akakereka?
Jibu: Amnasihi, amnasihi na kumwambia aondoke na asiswali na watu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ameamrisha usiswali na watu na kwamba aondoke nyumbani kwake na asiswali na watu na asile kitunguu saumu.
Swali: Lakini akate swalah yake na kwenda mahali pengine ikiwa ameshafunga swalah na anakereka na harufu hii na jambo hilo likamwathiri katika unyenyekevu wake?
Jibu: Ni jambo linahitaji kuangaliwa vyema. Akiweza kutoikata basi asiikate, kwa sababu imeshamuwajibiki kwa kule kuingia ndani yake. Katika hali hiyo inawamujibikia kuikamilisha. Kwa hivyo akiweza kujidhibiti aikamilishe.
Swali: Asipoweza na akaenda maeneo mengine?
Jibu: Ikiwezekana kwake kabla ya kukimiwa swalah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23792/ما-العمل-مع-من-وجد-به-راىحة-الثوم-بالمسجد
- Imechapishwa: 05/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)