Swali: Watu wengi wanaingia siku ya ijumaa wakati imamu anatoa Khutbah bila kuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti. Je, imamu awakemee…
Jibu: Sunnah ni kwamba wanatakiwa kuswali. Ambaye anaingia na imamu anatoa Khutbah anatakiwa kuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti. Ni lazima kwa imamu kuwakumbusha. Kwa ajili hiyo wakati Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alipomuona bwana mmoja aliyeingia na hakuswali swalah ya mamkuzi ya msikiti alimwambia:
“Simama na uswali Rak´ah mbili.”
Aliyafanya hayo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na huku anatoa Khutbah.
Swali: Ni wengi wanaofanya hivo. Amkumbushe kila mmoja anayeingia?
Jibu: Hapana, akumbushe kwa ujumla na watajua – Allaah akitaka. Kwa mfano awaambie kwamba anayeingia msikitini basi anapaswa kuswali Rak´ah mbili. Haijalishi kitu hata kama imamu anakhutubu awakumbushe mpaka lifike jambo la Allaah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22722/حكم-تحية-المسجد-اثناء-خطبة-الجمعة
- Imechapishwa: 02/08/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)