Imamu anasoma kwa sauti katika swalah za kusoma kimyakimya na kinyume chake

Swali: Je, waswaliji wanatakiwa kumzindua imamu pindi anaposoma kwa sauti katika swalah za kusoma kimyakimya au kinyume chake?

Jibu: Ndio. Akiendelea kusoma namna hiyo, wanatakiwa kumzindua.

Swali: Je, analazimika kuleta sujuud ya kusahau kwa ajili ya jambo hilo?

Jibu: Inapendeza. Halazimiki kufanya hivo, lakini inapendeza.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (40)
  • Imechapishwa: 21/05/2023