Ni ´Abdullaah bin az-Zubayr bin ´Iysaa bin ´Ubaydillaah bin Usaamah bin ´Abdillaah bin Humayd bin Zuhayr bin al-Haarith bin Asad bin ´Abd-il-´Uzza.
Kuna maoni yanayosema kuwa babu yake ni ´Iysaa bin ´Abdillaah bin az-Zubayr bin ´Ubaydillaah bin Humayd. al-Humaydiy ni Imaam, Haafidhw, Faqiyh na Shaykh wa Makkah; Abu Bakr al-Qurashiy, al-Asadiy, al-Humaydiy na al-Makkiy. Mtunzi wa “al-Musnad”.
Amehadithia kutoka kwa Ibraahiym bin Sa´d, Fudhwayl bin ´Iyaadhw na Sufyaan bin ´Uyaynah, ambaye alipokea sana kutoka kwake na akafanya vizuri, al-Waliyd bin Muslim, Marwaan bin Mu´aawiyah, Wakiy´ na ash-Shaafi´iy. Hakupokea sana lakini hata hivyo ana utukufu na heshima katika Uislamu.
Amehadithia kutoka kwake al-Bukhaariy, ad-Dhuhliy, Salamah bin Shu´ayb, Ya´quub al-Fasawiy, Abu Zur´ah ar-Raaziy, Bishr bin Muusa, Abu Haatim, Ya´quub bin Shaybah, Abu Bakr Muhammad bin Idriys al-Makkiy na alikuwa akiandika na wengineo.
Ahmad bin Hanbal amesema:
“Tunamzingatia al-Humaydiy kuwa imamu.”
Abu Haatim amesema:
“Mtu ambaye ni imara zaidi kwa Ibn ´Uyaynah ni al-Humaydiy. Yeye ndiye kiongozi wa wanafunzi wa Ibn ´Uyaynah. Ni imamu mwaminifu.”
Abu Ya´quub al-Fasawiy amesema:
“al-Humaydiy ametuhadithia na sijaona mtu ambaye anautakia Uislamu na waislamu kheri zaidi kuliko yeye.”
Muhammad bin Ishaaq al-Marwaziy amesema:
“Nimemsikia Ishaaq bin Raahuuyah akisema: “Maimamu katika zama zetu ni ash-Shaafi´iy, al-Humaydiy na Abu ´Ubayd.”
´Aliy bin Khalaf amesema:
“Nimemsikia al-Humaydiy akisema: “Hakuna yeyote atakayetushinda muda wa kuwa mimi niko Hijaaz, Ahmad bin Hanbal ´Iraaq na Ishaaq [bin Raahuuyah] Khuraasaan.”
Abul-´Abbaas as-Saraaj amesema:
“Nimemsikia Muhammad bin Ismaa´iyl akisema:
“al-Humaydiy ni imamu katika Hadiyth.”
Muhammad bin Sa´d amesema:
“´Abdullaah bin az-Zubayr al-Asadiy al-Humaydiy anatokana na kizazi cha Asad bin ´Abil-´Uzza bin Qusway, mwanafunzi wa Ibn ´Uyaynah na amepokea kwake, amekufa Makkah mwaka wa 219. Alikuwa mwaminifu na anayehifadhi sana.”
Vivyo hivyo ndivo alivosema al-Bukhaariy katika “Taariykh” kuhusu kufa kwake. Wengine wakasema kuwa amekufa mwaka wa 220.
Muslim amepokea kutoka kwake katika utangulizi wa kitabu chake, Ibn Maajah katika “at-Tafsiyr” na wengineo.
- Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (10/626-621)
- Imechapishwa: 13/09/2022
Ni ´Abdullaah bin az-Zubayr bin ´Iysaa bin ´Ubaydillaah bin Usaamah bin ´Abdillaah bin Humayd bin Zuhayr bin al-Haarith bin Asad bin ´Abd-il-´Uzza.
Kuna maoni yanayosema kuwa babu yake ni ´Iysaa bin ´Abdillaah bin az-Zubayr bin ´Ubaydillaah bin Humayd. al-Humaydiy ni Imaam, Haafidhw, Faqiyh na Shaykh wa Makkah; Abu Bakr al-Qurashiy, al-Asadiy, al-Humaydiy na al-Makkiy. Mtunzi wa “al-Musnad”.
Amehadithia kutoka kwa Ibraahiym bin Sa´d, Fudhwayl bin ´Iyaadhw na Sufyaan bin ´Uyaynah, ambaye alipokea sana kutoka kwake na akafanya vizuri, al-Waliyd bin Muslim, Marwaan bin Mu´aawiyah, Wakiy´ na ash-Shaafi´iy. Hakupokea sana lakini hata hivyo ana utukufu na heshima katika Uislamu.
Amehadithia kutoka kwake al-Bukhaariy, ad-Dhuhliy, Salamah bin Shu´ayb, Ya´quub al-Fasawiy, Abu Zur´ah ar-Raaziy, Bishr bin Muusa, Abu Haatim, Ya´quub bin Shaybah, Abu Bakr Muhammad bin Idriys al-Makkiy na alikuwa akiandika na wengineo.
Ahmad bin Hanbal amesema:
“Tunamzingatia al-Humaydiy kuwa imamu.”
Abu Haatim amesema:
“Mtu ambaye ni imara zaidi kwa Ibn ´Uyaynah ni al-Humaydiy. Yeye ndiye kiongozi wa wanafunzi wa Ibn ´Uyaynah. Ni imamu mwaminifu.”
Abu Ya´quub al-Fasawiy amesema:
“al-Humaydiy ametuhadithia na sijaona mtu ambaye anautakia Uislamu na waislamu kheri zaidi kuliko yeye.”
Muhammad bin Ishaaq al-Marwaziy amesema:
“Nimemsikia Ishaaq bin Raahuuyah akisema: “Maimamu katika zama zetu ni ash-Shaafi´iy, al-Humaydiy na Abu ´Ubayd.”
´Aliy bin Khalaf amesema:
“Nimemsikia al-Humaydiy akisema: “Hakuna yeyote atakayetushinda muda wa kuwa mimi niko Hijaaz, Ahmad bin Hanbal ´Iraaq na Ishaaq [bin Raahuuyah] Khuraasaan.”
Abul-´Abbaas as-Saraaj amesema:
“Nimemsikia Muhammad bin Ismaa´iyl akisema:
“al-Humaydiy ni imamu katika Hadiyth.”
Muhammad bin Sa´d amesema:
“´Abdullaah bin az-Zubayr al-Asadiy al-Humaydiy anatokana na kizazi cha Asad bin ´Abil-´Uzza bin Qusway, mwanafunzi wa Ibn ´Uyaynah na amepokea kwake, amekufa Makkah mwaka wa 219. Alikuwa mwaminifu na anayehifadhi sana.”
Vivyo hivyo ndivo alivosema al-Bukhaariy katika “Taariykh” kuhusu kufa kwake. Wengine wakasema kuwa amekufa mwaka wa 220.
Muslim amepokea kutoka kwake katika utangulizi wa kitabu chake, Ibn Maajah katika “at-Tafsiyr” na wengineo.
Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (10/626-621)
Imechapishwa: 13/09/2022
https://firqatunnajia.com/imaam-al-humaydiy/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)