Swali: Baadhi ya watu hufanya Idhwtibaa´ katika swalah?

Jibu: Hapana, haifai kufanya Idhtibaa´ katika swalah. Bali anatakiwa kuivaa nguo yake juu ya mabega yake. Idhwtibaa´ hufanywa katika Twawaaf ya kuwasili tu. Ama katika sehemu nyingine isiyokuwa Twawaaf ya kuwasili, basi anatakiwa kuivaa juu ya mabega yake yote mawili.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/346)
  • Imechapishwa: 14/03/2026