Swali: Kuna mtu alikuwa anaamini kuwa kufanya jimaa mchana wa Ramadhaan pasi na kumwaga hakuharibu swawm. Ana nini juu yake?
Jibu: Ikiwa aina ya mtu kama huyu kweli hajui, bi maana si msomi kihakika na hakuwahi kusikia kupata elimu yoyote kwamba tendo hili linaharibu swawm, swawm yake ni sahihi na haikuharibika na kadhalika haimlazimu yeye kulipa kama jinsi haimlazimu kutoa kafara. Ama ikiwa aina ya mtu kama huyu anajua, kwa mfano aliwahi kusoma na akajua au alisikia kwa watu, hana udhuru. Muhimu ni kwamba, ikiwa ni mkweli kwa ujinga wake na aina kama yeye hajui, hana lolote juu yake, si kulipa, kafara wala madhambi. Allaah (Ta´ala) amesema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Mola wetu usituchukulie tukisahau au tukikosea.” (02:286)
Vilevile Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) katika zama za Mtume walikula wakati walipofikiria kuwa jua limeshazama halafu baada ya hapo jua likachomoza, hata hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwaamrisha kulipa kwa kuwa hawakuwa wanajua wakati. Kula na kunywa ni kama jimaa, hakuna tofauti kati yake kwa sababu yote mawili yanaharibu swawm. Ikiwa swawm haiharibiki kwa kula pasi na mtu kujua, kadhalika jimaa.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 02
- Imechapishwa: 23/09/2020
Swali: Kuna mtu alikuwa anaamini kuwa kufanya jimaa mchana wa Ramadhaan pasi na kumwaga hakuharibu swawm. Ana nini juu yake?
Jibu: Ikiwa aina ya mtu kama huyu kweli hajui, bi maana si msomi kihakika na hakuwahi kusikia kupata elimu yoyote kwamba tendo hili linaharibu swawm, swawm yake ni sahihi na haikuharibika na kadhalika haimlazimu yeye kulipa kama jinsi haimlazimu kutoa kafara. Ama ikiwa aina ya mtu kama huyu anajua, kwa mfano aliwahi kusoma na akajua au alisikia kwa watu, hana udhuru. Muhimu ni kwamba, ikiwa ni mkweli kwa ujinga wake na aina kama yeye hajui, hana lolote juu yake, si kulipa, kafara wala madhambi. Allaah (Ta´ala) amesema:
رَبَّنَا لَا تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا
“Mola wetu usituchukulie tukisahau au tukikosea.” (02:286)
Vilevile Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) katika zama za Mtume walikula wakati walipofikiria kuwa jua limeshazama halafu baada ya hapo jua likachomoza, hata hivyo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuwaamrisha kulipa kwa kuwa hawakuwa wanajua wakati. Kula na kunywa ni kama jimaa, hakuna tofauti kati yake kwa sababu yote mawili yanaharibu swawm. Ikiwa swawm haiharibiki kwa kula pasi na mtu kujua, kadhalika jimaa.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Kanda “Liqaa´aatu Ramadhwaaniyyah”, sehemu ya 02
Imechapishwa: 23/09/2020
https://firqatunnajia.com/ibn-uthaymiyn-mfungaji-aliyemjamii-mke-wake-akifikiria-kuwa-inajuzu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)