Jopo la wanachuoni wengi wanaona kuwa kuchinja katika ´Iyd-ul-Adhwhaa imependekezwa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo na akahimiza kitendo hicho na Ibn ´Abbaas ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Nimeamrishwa mambo matatu na yamependekezwa juu yenu; Witr, kuchinja na Rak´ah mbili kabla ya Fajr.”
Ameipokea ad-Daaraqutwniy.
Ahmad anayo maoni mengine yanayosema kuwa ni wajibu. Haya pia ndio maoni ya Abu Bakr [´Abdul-´Aziyz]. Hayo ni kutokana na maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye nafasi na asichinje basi asisogelee uwanja wetu wa kuswalia.”[1]
Anayo maoni ya tatu yanayosema kuwa si wajibu isipokuwa kwa yule ambaye si msafiri.
Yuko na maoni mengine yanayosema kwamba ikiwa mtu yuko mwenye wepesi anatakiwa kuchinja. Hapa ndipo Abul-Khattwaab akaelewa kuwa ni lazima. Lakini hata hivyo mambo sivyo. Kwa sababu suala linahusiana na wepesi, na si kwamba kitendo hicho ni lazima.
[1] Ahmad (1/321), Ibn Maajah (3123), ad-Daaraqutwniy (2/545) na al-Haakim (4/231).
- Mhusika: Imaam Ibraahiym bin Muhammad al-Maqdisiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Mubdi´ (3/297)
- Imechapishwa: 11/07/2020
Jopo la wanachuoni wengi wanaona kuwa kuchinja katika ´Iyd-ul-Adhwhaa imependekezwa. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo na akahimiza kitendo hicho na Ibn ´Abbaas ameeleza kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Nimeamrishwa mambo matatu na yamependekezwa juu yenu; Witr, kuchinja na Rak´ah mbili kabla ya Fajr.”
Ameipokea ad-Daaraqutwniy.
Ahmad anayo maoni mengine yanayosema kuwa ni wajibu. Haya pia ndio maoni ya Abu Bakr [´Abdul-´Aziyz]. Hayo ni kutokana na maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule mwenye nafasi na asichinje basi asisogelee uwanja wetu wa kuswalia.”[1]
Anayo maoni ya tatu yanayosema kuwa si wajibu isipokuwa kwa yule ambaye si msafiri.
Yuko na maoni mengine yanayosema kwamba ikiwa mtu yuko mwenye wepesi anatakiwa kuchinja. Hapa ndipo Abul-Khattwaab akaelewa kuwa ni lazima. Lakini hata hivyo mambo sivyo. Kwa sababu suala linahusiana na wepesi, na si kwamba kitendo hicho ni lazima.
[1] Ahmad (1/321), Ibn Maajah (3123), ad-Daaraqutwniy (2/545) na al-Haakim (4/231).
Mhusika: Imaam Ibraahiym bin Muhammad al-Maqdisiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Mubdi´ (3/297)
Imechapishwa: 11/07/2020
https://firqatunnajia.com/ibn-muflin-kuhusu-hukumu-ya-kuchinja-katika-iyd-ul-adhwhaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)