Swali: Vipi kwa mfungaji ambaye amekula hali ya kuwa amesahau?
Jibu: Hakuna kinachomlazimu. Hana kafara wala kulipa.
Swali: Vipi akifanya tendo la ndoa kwa kusahau?
Jibu: Sahihi ni kwamba funga yake ni sahihi. Isitoshe halazimiki kutoa kafara. Baadhi ya wanazuoni wamebagua jimaa. Hata hivyo hakuna dalili juu ya hilo. Kwa ajili hiyo imekuja katika tamko jengine:
”Anayefungua katika Ramadhaan kwa kusahau hakuna juu yake kulipa wala kafara.”
Swali: Vipi nikimuona anakunywa kwa kusahau?
Jibu: Mkumbushe, kwa sababu ni maasi. Ukimuona anayekunywa au anayekula ndani ya swawm yake, mkumbushe na kumwambia kuwa amefunga. Mweleze na umkataze.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24412/حكم-الصاىم-اذا-اكل-او-شرب-او-جامع-ناسيا
- Imechapishwa: 07/10/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)