Swali: Je, kuna tatizo katika kufasiri neno nafsi kwa maana ya dhati katika haki ya Allaah (´Azza wa Jall)?
Jibu: Sijui kizuizi chochote kuhusu ya hilo. Linaweza kufasiriwa kuwa dhati na linaweza pia kuwa na maana nyingine maalum zaidi kuliko dhati. Maana inayoonekana katika dalili za Qur-aan na Hadiyth inajumuisha dhati na pia maana nyingine, kama alivyosema (´Azza wa Jall):
تَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِي وَلَا أَعْلَمُ مَا فِي نَفْسِكَ
”Unayajua yale yote yaliyomo katika nafsi yangu na wala [mimi] sijui yale yaliyomo katika Nafsi Yako.”[1]
Hii ni kwa namna inavyomstahiki Allaah. Hakuna ajuaye namna ilivyo isipokuwa Yeye tu (´Azza wa Jall).
[1] 5:116
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25299/ما-حكم-تفسير-النفس-لله-عز-وجل-بالذات
- Imechapishwa: 25/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)