Swali: Ni lini inaanza swalah ya kupatwa kwa jua?
Jibu: Ataanza kuswali kuanzia pale atapoona kupatwa kwa jua. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtapoona hilo basi swalini!”
Swali: Maneno yake aliposema:
“Swalini Rak´ah mbili kwa Rukuu´ mbili.”
si kunafahamisha kuwa Rukuu´ ya pili ni ukamilifu wa Rukuu´ ya kwanza?
Jibu: Rukuu´ mbili katika kila Rak´ah. Kila Rak´ah moja inayo Rukuu´mbili, Sujuud mbili na visomo viwili. Na kila kisomo pamoja na al-Faatihah.
Swali: Je, kumepokelewa kitu kuhusu kwamba kupatwa kwa jua inatokana na madhambi?
Jibu: Imepokelewa katika Hadiyth Swahiyh ambayo amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Khutbah yake:
“Hakuna yeyote mwenye wivu zaidi kuliko Allaah ambapo akazini mja wake au akazini mjakazi wake.”
Uzinzi ni miongoni mwa ghadhabu za Allaah (´Azza wa Jall) na ni miongoni mwa sababu za hasira pale kunapotangaa uzinzi na machafu. Tunamuomba Allaah usalama. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hakuna yeyote mwenye wivu zaidi kuliko Allaah.”
Kwa ajili hiyo akaharamisha machafu yenye kuonekana na yenye kujificha.
Swali: Je, inafaa kwake kusoma ndani ya msahafu?
Jibu: Inafaa kwake kusoma ndani ya msahafu akiwa na hifdhi. Vinginevyo asome ndani ya msahafu.
Swali: Rukuu´ ya pili ni wajibu au Sunnah?
Jibu: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alifanya hivo. Ni wajibu kufanya kama alivofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Isitoshe amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”
Swali: Je, watu wa mashambani wasiojua zaidi ya al-Faatihah wajishughulishe na kufanya Dhikr peke yake?
Jibu: Waswalini na wasome al-Faatihah na himdi zote njema anastahiki Allaah.
Swali: Je, mtu alipe Rak´ah nyingine akikosa Rukuu´ ya kwanza?
Jibu: Ndio. Akikosa Rukuu´ ya kwanza alipe Rak´ah nyingine, kwani akikosa Rukuu´ ya kwanza amekosa Rak´ah.
Swali: Baadhi ya maimamu wanategemea juu ya kuswali kwao vyombo vya khabari…
Jibu: Ni lazima kuona [kupatwa kwa mwezi]. Khabari za wahasibu hazifanyiwi kazi. Kinachotegemewa ni kuona. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mtapoona hilo basi swalini!”
Hakusema watu wakisikia au watu wakijua. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mtapoona kupatwa kwa jua.”
Kutegemea hesabu hapana.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23886/حكم-صلاة-الكسوف-وبدايتها-وكيفيتها
- Imechapishwa: 27/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)