Swali: Aligeukie jiwe mwili mzima…?
Jibu: Analielekee, alielekee na kulibusu ikiwa itawezekana. Na kama akilipa upande wake na kuligusa, hakuna shida, jambo hili ni pana.
Swali: Vipi kuongeza:
بسم الله
”Kwa jina la Allaah.”?
Jibu: Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) ndiye alikuwa akifanya hivo. Jambo ni lenye wasaa. Lakini sijui chochote sahihi na kuthibiti. Ni katika matendo ya Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa).
Swali: Katika mizunguko yote au mzunguko wa kwanza tu?
Jibu: Katika mizunguko yote, kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho. Kila anapokaribia jiwe, basi alete Takbiyr kisha aendelee.
Swali: Je, kuna chochote kumepokelewa kuhusu kusujudu juu ya jiwe?
Jibu: Imepokewa katika baadhi ya Hadiyth kuhusu kusujudu juu ya jiwe. Hakuna ubaya kufanya hivyo. Kuna Hadiyth kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na zenye kuishilia kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) kuhusu jambo hilo. Lakini Hadiyth zilizothibiti zinaeleza kuhusu kubusu. Kwa hivyo inatosha kubusu.
Swali: Kusema:
بسم الله
”Kwa jina la Allaah.”
katika mzunguko wa kwanza ni katika matendo ya Ibn ´Umar?
Jibu: Ndio, alikuwa akifanya hivyo Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh). Udhahiri ni kwamba alikuwa akifanya hivyo katika kila mzunguko. Ama Hadiyth zilizothibi zinataja tu Takbiyr.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24983ما-يصح-وما-لا-يصح-في-استقبال-الحجر-الاسود
- Imechapishwa: 20/01/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket