Hukumu ya watu watakaomwamini al-Masiyh ad-Dajjaal

Swali: Kila ambaye atapewa mtihani wa ad-Dajjaal ataingia Motoni na kudumishwa ndani yake?

Jibu: Akimkufuru Allaah na akafa katika ukafiri wake ni katika watu wa Motoni. Ama akitubu na kurejea kwa Allaah, Allaah Atamsamehe. Huyu ni kama wapotevu wengine ambao wataritadi kisha warudi [katika Uislamu]. Mwenye kutubu Allaah Humsamehe. Kuhusu mwenye kufa baada ya kuritadi na juu ya ukafiri, huyu ni katika watu wa Motoni.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kitaab Ahaadiyth-il-Fitnah http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/hadist%20fitan-17-08-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 21/04/2015