Swali: Nawaona baadhi ya waswaliji wanaweka ncha ya vilemba vyao chini ya paji zao za uso wakati wamesujudu. Ni ipi hukumu ya kitendo chao hichi?
Jibu: Ikiwa haja imepelekea kufanya hivo, kwa mfano ardhi ni yenye baridi, joto kali au kufunika uchi wake, hapana neno kufanya hivo. Maswahabah wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakifanya hivo wakati wa haja. Lakini kukiwa hakuna haja bora ni kutofanya hivo na mswaliji abashiri ardhi kwa uso wake. Hivo ndivo alivokuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akifanya na Maswahabah zake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/158)
- Imechapishwa: 23/10/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket