Hekima ya kujenga misikiti na kuzuia ujenzi wa makanisa nchini mwetu

Swali: Vipi kumraddi anayesema kuwa ni kwa nini haturuhusu kujenga makanisa kwetu kama wao wanavyoturuhusu kujenga misikiti katika miji yao?

Jibu: Misikiti ni haki. Ni nyumba za Allaah. Kuhusu makanisa ni batili. Ni vipi tuwaruhusu kusimamisha batili katika nchi yetu? Misikiti ni haki. Hilo ndio la wajibu kwa watu wa ardhini, kwa sababu ni nyumba za Allaah. Sisi tunafanyia kazi haki na tunazuia batili. Lakini ikiwa kuna mkataba wa amani kati yetu sisi na wao, tunawaachia makanisa yao ambayo tayari yapo ili wafanye ´ibaadah zao ndani yake na wasizidhihirishe. Ama kuanza kujenga makanisa mapya ni jambo limekatazwa na khaswa katika kisiwa cha kiarabu ambacho ndio kitovu cha Ujumbe na chanzo cha Uislamu. Hakutakiwi kubaki dini mbili, kama alivosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hakuna kinachotakiwa kubaki isipokuwa Uislamu peke yake ili haki isichanganyikane na batili. Hii ndio hekima ya kutowaacha kujenga makanisa, kwa sababu ni batili. Lakini sisi tunajenga misikiti kwao kwa sababu ni haki. Misikiti ni nyumba za Allaah (´Azza wa Jall). Sio nyumba zetu sisi. Ni nyumba za Allaah (´Azza wa Jall).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ta´liyqaat ´alaa Risaalah wujuub-il-´Amr bil-Ma´ruuf wan-Nahiy ´an al-Munkar (01)
  • Imechapishwa: 31/01/2024