Hawa ndio wenye kufananisha sifa za Allaah na viumbe

Imaam at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:

“Hakuna katika viumbe aliyefanana na Yeye”

Mwandishi amechokusudia ni kuwaraddi Mushabbihah ambao wanamfananisha Allaah na viumbe Wake. Wamevuka mipaka katika kuthibitisha. Wanasema kuwa elimu ya Allaah ni kama elimu ya viumbe, uwezo Wake ni kama uwezo wao, usikivu Wake ni kama usikivu wao na kulingana Kwake ni kama kulingana kwao. Haya ndio madhehebu ya Mushabbihah.

Mara nyingi Mushabbihah wanakuwa katika Shiy´ah walopetuka mipaka. Mtu wa kwanza aliyesema kuwa Allaah ana mwili ni Hishaam bin al-Hakam ar-Raafidhwiy na Bayaan bin Sim´aan at-Tamiymiy. Mtu huyu alikuwa anasema kuwa Allaah yuko na sura ya mwanaadamu.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/64)
  • Imechapishwa: 01/06/2020