Hapo ndipo utapotoa Zakaat-ul-Fitwr yako

Swali: Mtu akiwa katika safari na akatoa Zakaat-ul-Fitwr yake ndani ya wakati wake katika nchi aliyoko kabla ya kufika nyumbani kwake. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Hapana vibaya kufanya hivo hata kama atakuwa mbali na watoto wake. Kwani Zakaat-ul-Fitwr inatolewa pale pahali ambapo imekuwajibikia ukiwa maeneo hapo ingawa ni mbali na mji wako.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/263)
  • Imechapishwa: 26/04/2026