Hapo ndipo itamlazimu mume kumhudumia

Swali: Mwanaume amemuoa mwanamke ambapo akabaki kwa familia yake mwaka mzima kabla ya kufanya sherehe ya ndoa na kuhama pamoja. Je, analazimika kumhudumia katika kipindi hicho?

Jibu: Hapana. Asimuhudumie mpaka wahame pamoja. Muda wa kuwa hawajahama pamoja na sababu ni kutoka kwake yeye au familia yake, basi hakuna kinachomlazimu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (37)
  • Imechapishwa: 28/07/2023