Swali: Baadhi ya wanafunzi wanakosoa baadhi ya makosa ya wanachuoni ambapo baadae wanayaeneza kati ya watu na wanasema kuwa ni Jarh na Ta´diyl. Je, kitendo chake ni sahihi?
Jibu: Mmekariri swali hili kuhusu Jarh na Ta´diyl. Jarh na Ta´diyl ni elimu kuhusu mlolongo wa wapokezi wa Hadiyth. Jarh na Ta´diyl haiwahusu watu wasiopokea Hadiyth na wala hawana mafungamano yoyote na Hadiyth. Huku ni kusengenya na kueneza uvumi. Sio Jarh na Ta´diyl. Huku ni kusengenya ambako hakujuzu. [Inajuzu tu] ikiwa mtu huyu madhara yake ni yenye kuenea kwa wengine na anasababisha wengine kupotea. Katika hali hii ni wajibu kubainisha hali yake na kutahadharisha nae.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Furqaan (07) http://alfawzan.af.org.sa/node/2050
- Imechapishwa: 27/12/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket