Swali: Kuna muislamu amemwambia ndugu yake kuwa ni kafiri pamoja na kuwa aliyeambiwa hivyo anaswali vipindi vitano na kuswali. Ni ipi hukumu na ni ipi dawa ya kusahau sana?
Jibu: Haijuzu kwa muislamu kumpachika ndugu yake kufuru ikiwa hakufanya kitu hicho. Ni wajibu kwake kutubu na kumuomba msamaha Allaah pamoja na kumtaka radhi ndugu yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametishia hilo katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh.
Kuhusu namna ya kutibu kusahau na kuhifadhi ni kumcha Allaah (´Azza wa Jall), kudumu kwa kurejelea na kukariri vile unavyotaka kuvihifadhi. Pamoja na kumuomba Allaah akusaidie juu ya hilo. Tunamuomba Allaah akupe wewe na sisi mafanikio katika kuhakikisha yale uliyoyakusudia.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (2/91)
- Imechapishwa: 24/08/2020
Swali: Kuna muislamu amemwambia ndugu yake kuwa ni kafiri pamoja na kuwa aliyeambiwa hivyo anaswali vipindi vitano na kuswali. Ni ipi hukumu na ni ipi dawa ya kusahau sana?
Jibu: Haijuzu kwa muislamu kumpachika ndugu yake kufuru ikiwa hakufanya kitu hicho. Ni wajibu kwake kutubu na kumuomba msamaha Allaah pamoja na kumtaka radhi ndugu yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametishia hilo katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh.
Kuhusu namna ya kutibu kusahau na kuhifadhi ni kumcha Allaah (´Azza wa Jall), kudumu kwa kurejelea na kukariri vile unavyotaka kuvihifadhi. Pamoja na kumuomba Allaah akusaidie juu ya hilo. Tunamuomba Allaah akupe wewe na sisi mafanikio katika kuhakikisha yale uliyoyakusudia.
Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (2/91)
Imechapishwa: 24/08/2020
https://firqatunnajia.com/haijuzu-kwa-yeyote-kuwakufurisha-waislamu/