Swali: Kuna muislamu amemwambia ndugu yake kuwa ni kafiri pamoja na kuwa aliyeambiwa hivyo anaswali vipindi vitano na kuswali. Ni ipi hukumu na ni ipi dawa ya kusahau sana?
Jibu: Haijuzu kwa muislamu kumpachika ndugu yake kufuru ikiwa hakufanya kitu hicho. Ni wajibu kwake kutubu na kumuomba msamaha Allaah pamoja na kumtaka radhi ndugu yake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametishia hilo katika Hadiyth ambazo ni Swahiyh.
Kuhusu namna ya kutibu kusahau na kuhifadhi ni kumcha Allaah (´Azza wa Jall), kudumu kwa kurejelea na kukariri vile unavyotaka kuvihifadhi. Pamoja na kumuomba Allaah akusaidie juu ya hilo. Tunamuomba Allaah akupe wewe na sisi mafanikio katika kuhakikisha yale uliyoyakusudia.
- Muhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Lajnah ad-Daaimah (2/91)
- Imechapishwa: 24/08/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket