Swali: Ambaye atafanya I´tikaaf siku moja kwa ajili ya Allaah basi Allaah atafanyia baina yake na Moto mahandaki matatu?
Jibu: Hadiyth hii ni dhaifu. Hadiyth kuhusu fadhilah za I´tikaaf zote ni dhaifu. Kilichothibiti ni kwamba inapendeza. Kitendo cha yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba alifanya I´tikaaf ndio kilichothibiti. Vilevile maneno Yake (Jalla wa ´Alaaa):
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ
“Na wala msichanganyike nao hali ya kuwa nyinyi ni wenye kukaa I’tikaaf misikitini.”[1]
Huu ndio msingi. Ama Hadiyth kuhusu fadhilah za I´tikaaf hatujui ambayo ni Swahiyh.
[1] 02:187
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22840/هل-صحت-احاديث-في-فضل-الاعتكاف
- Imechapishwa: 08/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)