Du´aa za pamoja baada ya swalah za faradhi ni Bid´ah

Swali: Je, du´aa ya imamu na maamuma kusema “Aamiyn” baada ya swalah ya faradhi ni katika Bid´ah? Je, inajuzu kuinua mikono katika dua ya Qunuut?

Jibu: Kuwa imamu anafanya du´aa baada ya swalah tano za faradhi na maamuma wanaitikia “Aamiyn”, hili ni Bid´ah na halina asili. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakulifanya na wala Maswahabah wake hawakulifanya. Imamu anapotoa salamu na maamuma pia, kila mmoja ashughulike na kumtaja Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Ama imamu kuinua mikono na kuomba du´aa na wengine kuitikia “Aamiyn”, hili halina msingi na ni katika Bid´ah.

Ama Qunuut, hilo ni jambo lililowekwa katika Shari´ah na kuinua mikono katika Qunuut ni jambo limesuniwa. Imethibiti kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiinua mikono yake katika Qunuut wakati wa misiba na Qunuut ya witr ni kama hiyo, sawa na Qunuut ya majanga.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3304/حكم-الدعاء-بعد-الفريضة-ورفع-اليدين-في-القنوت
  • Imechapishwa: 08/08/2026