Swali: Baada ya imamu kusoma Suurah “adh-Dhuhaa” katika Tarawiyh, aliwaamrisha waswaliji kusema kwa sauti:
لا إِلهَ إِلاَّ الله
“Hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah.”
الله أَكبر
“Allaah ni mkubwa.”
الْحَمْدُ لله
“Himdi zote njema anastahiki Allaah.”
Anadai kuwa ni Sunnah na kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaamrisha Maswahabah zake kumshukuru Allaah wakati uliposimama wahy. Ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Ni kweli ipo Hadiyth katika jambo hilo, lakini ni dhaifu. Haafidhw adh-Dhahabiy ameitaja katika “Twabaqaat-ul-Qurraa´ al-Kibaar” na akasema kuwa katika cheni yake ya wapokezi yuko Abiy Bazzah. Sio al-Qaasim bin Abiy Bazzah, isipokuwa mjukuu wake Ahmad bin Muhammad. Kwa hivyo Hadiyth haikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa maana nyingine ni Bid´ah kusema hivo.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 311-312
- Imechapishwa: 11/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket