Swali: Asiyetahiri anapata dhambi?

Jibu: Wanazuoni wengi wanaona kuwa inapendeza. Ahmad (Rahimahu Allaah), Ibn ´Abbaas na kikosi cha wanazuoni wengine wanaona kuwa ni wajibu.

Swali: Asiyetahiri anapata dhambi?

Jibu: Wale ambao wanaona kuwa ni wajibu anapata dhambi. Wale ambao wanaona kuwa inapendeza hapati dhambi. Hata hivyo mtu anatakiwa kufanya hivo, kama alivosema Ibn ´Abbaas na akatilia mkazo wa hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaambia baadhi ya Maswahabah waliposilimu:

”Ondosha nywele za ukafiri na tahiri!”

Hata hivyo katika cheni ya upokezi kuna unyonge.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24282/هل-ياثم-من-لم-يختتن
  • Imechapishwa: 23/09/2024