Swali: Je, swalah ya ijumaa inatosheleza kwa wanawake?

Jibu: Akiihudhuria ataiswali ijumaa. Vinginevyo ataiswali nyumbani hali ya kuwa Dhuhr. Wanawake hawana swalah ya ijumaa. Lakini wakihudhuria swalah ya ijumaa inasihi. Wasipohudhuria wataiswali hali ya kuwa ni Dhuhr Rak´ah nne majumbani mwao. Ni kama mfano wa mgonjwa anatakiwa kuswali Dhuhr nyumbani. Mwanamke pia ataiswali Dhuhr nyumbani. Kuiswali nyumbani ndio bora:

“Majumba yao ndio bora kwao.”

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23493/هل-تجزى-الجمعة-عن-الظهر-للمراة
  • Imechapishwa: 28/01/2024