Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“… na kila upotevu ni Motoni.”
Kila kitakachozushwa ni Bid´ah na uvumbuzi unaoipoteza dini ya Allaah. Wenye kufanya hivi hawana jengine zaidi ya Moto ikiwa Allaah Hakuwasamehe na wakatubu kwa Allaah (Tabaarak wa Ta´ala).
Mifumo ya upotevu inaongoza katika Moto na tunaomba kinga kwa Allaah. Kadhalika Bid´ah inawaongoza watu wake katika Moto. Upande mwingine Kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) vinaongoza katika Pepo:
وَاللَّـهُ يَدْعُو إِلَىٰ دَارِ السَّلَامِ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ
“Allaah anaitia nyumba ya amani na Anamwongoza Amtakaye kuelekea njia iliyonyooka.” (10:25)
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: adh-Dhariy´ah ilaa Bayaan Maqaaswid Kitaab-ish-Sharï´ah (1/219)
- Imechapishwa: 26/08/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)