Swali: Ni jambo la kupindukia kufuata kipofu moja katika madhehebu mane?
Jibu: Hapana. Mtu ambaye si msomi na ambaye anaanza sasa hawezi jengine zaidi ya kufuata kipofu. Vinginevyo afanye nini? Afanye Ijtihaad mwenyewe? Hana uwezo wa kufanya Ijtihaad. Awafuate wanachuoni. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
فَاسْأَلُوا أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ
“Waulizeni watu wenye kumbukumbu Ukumbusho ikiwa hamjui.” (16:43)
Kwa nini wawaulize? Ili wafuate yale wanayoyasema. Kufuata kichwa mchunga inakuwa kwa sababu ya dharurah na haja. Ambaye hana uwezo wa kutafiti dalili na kuonelea usawa awafuate wanachuoni:
فَاسْأَلُوا أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ
“Waulizeni watu wenye kumbukumbu Ukumbusho ikiwa hamjui.” (16:43)
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (35) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighasah%20%20-%2017-%2010-1436.mp3
- Imechapishwa: 12/02/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket