Swali 380: Ni ipi hukumu kwa mwenye kuswali Sunnah ya kabla ya Fajr nyumbani kwake kisha akaingia msikitini na akawakuta watu hawajasimama kwa ajili ya swalah. Je, aswali Tahiyyat-ul-Masjid kwa sababu ni miongoni mwa mambo vyenye sababu au abaki akiwa ni mwenye kusubiri bila ya kuswali?
Jibu: Jambo ni lenye wasaa. Akibaki ni mwenye kusimama mpaka kukakimiwa swalah ni sawa. Akikusudia kwa swalah ile Tahiyyat-ul-Masjid na akapenda kubaki akiwa ni mwenye kusimama na asikae chini… kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Atapoingia mmoja wenu msikitini basi asikae chini mpaka arukuu Rak´ah mbili.”
pia ni sawa. Akipenda kurukuu Tahiyyat-ul-Masjid na kwayo akanuia Tahiyyat-ul-Masjid pia inafaa. Inazingatiwa ni miongoni mwa vyenye sababu. Allaah ndiye mjuzi zaidi.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ijaabatu as-Saa-il, uk. 637
- Imechapishwa: 13/12/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)