Swali: Je, ni lazima kwa mwanamke kufumua nywele zake wakati wa kujitwahirisha na hedhi?
Jibu: Hapana, inapendeza tu. Kwa ajili hiyo imekuja katika Hadiyth ya Umm Salamah iliyopokelewa na Muslim ambaye aliuliza:
“Je, nizifungue ninapotoka kwenye hedhi?” Akamjibu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Hapana. Hapana vyenginevyo inakutosha kuzimiminia maji.”
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24761/حكم-نقض-الشعر-لغسل-الحيض
- Imechapishwa: 07/12/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)
Related
Aache kuoga josho la hedhi na janaba kwa sababu ya nywele kupukuchika wakati wa kuziosha?
Swali: Kuna mwanamke amepatwa na maradhi yanayofanya nywele zake kupukuchipa wakati anapoziosha na maji. Afanye nini? Je, aache kuoga josho la hedhi na janaba? Jibu: Hapana, ni lazima aoge kwa ajili ya hedhi na janaba. Nywele kupukuchika kwa kuzitia maji ni ugonjwa na maradhi. Itambulike kuwa Allaah hakuteremsha ugonjwa wowote…
In "Matibabu"
15. Hukumu ya kumi: Mafungamano ya hedhi na kuoga
10- Ni wajibu kwa mwanamke mwenye hedhi pale anapotwaharika kuosha mwili wake wote. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kumwambia Faatwimah bint Abiy Hubaysh: "Wakati hedhi inapokuja acha swalah. Pindi hedhi yako inapoisha jisafishe na uswali."[1] Uwajibu wa chini kabisa katika kuoga ni kulowa mwili mzima ikiwa ni pamoja…
In "ad-Dimaa' at-Twabiy´iyyah lin-Nisaa' - Damu ya kimaumbile ya wanawake"