Swali: Mtu ambaye ana deni la swawm ya Ramadhaan – je, inajuzu kwake kufunga swawm za kujitolea na khaswa ikiwa ni katika siku ambazo fadhilah zake hupitwa, kama siku ya ´Aashuuraa´ au siku ya ´Arafah?

Jibu: Hapana. Bali alipe kwanza swawm ya faradhi, kwa sababu faradhi inatangulizwa. Ikiwa anataka kufunga siku ya ´Arafah au ´Aashuuraa´, basi afunge swawm ya faradhi kabla yake. Ikiwa atafunga siku ya ´Aashuuraa´ kwa nia ya kulipa swawm ya faradhi, basi inamtosheleza kuwa ni malipo ya faradhi.

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (24)
  • Imechapishwa: 16/09/2026