Anakufuru mwenye kutilia shaka ukafiri wa washirikina?

Swali: Je, yule mwenye kutilia shaka ukafiri wa washirikina moyoni mwake na asitamke hilo kwa ulimi wake anakufuru? Ipi tofauti kati ya hili na mazungunzo ya kuizungumzisha nafsi?

Jibu: Shaka inakuwa moyoni. Akitilia shaka moyoni kuhusu washirikina kama ni makafiri kweli au si makafiri, anaritadi kwa hilo. Akitamka basi jambo lina ukhatari zaidi. Ama mazungumzo ya kuizungumzisha nafsi pasi na kutilia shaka hayadhuru.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 95-96
  • Imechapishwa: 21/09/2018