Anajiwa na kiumbe usingizini kinachomuamrisha kufanya mambo kadhaa

Swali: Mwanamke huyu amemuona ndotoni Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa umbo na wasifu wake pamoja na Abu Bakr (Radhiya Allaahu Allaahu ´anh), hata hivyo Abu Bakr alikuwa ni mrefu zaidi kuliko Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwenye ndoto nyingine amesikia simu anapigiwa na akadhania kuwa ni Malaika ambapo akamfunza mwisho wa Suurat-ul-Baqarah. Kiumbe hicho kikamwambia awasomee nayo wanawake na awatemee cheche za mate na Allaah atanufaisha watu kupitia wewe. Mwanamke huyo anasema akaanza kuwasomea wanawake na wengi wao wakanufaika…

Jibu: Usisadikishe kiumbe hicho. Inawezekana ikawa ni shaytwaan anataka kumdanganya. Aachane na kitendo hichi na wala asikiendekeze. Mwenye kukuamrisha [usingizini] na kukwambia ufanye kitu fulani, hili haliwi isipokuwa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Isitoshe hakuna yeyote awezae kuamrisha na kukataza [ndotoni] baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Qaa´idah Jaliylah fiyt-Tawassul wal-Wasiylah (30) http://alfawzan.af.org.sa/node/2142