Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah hatazami miili yenu wala mali zenu; anatazama nyoyo zenu na matendo yenu.”[1]
Nini makusudio ya kutokutazama?
Jibu: Makusudio ya kutokutazama ni kwamba hatilii umuhimu wowote. Hadiyth hii ni kama mfano wa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Allaah hatowatazama siku ya Qiyaamah na wala hatowatakasa.”[2]
Kwa sababu ya kuwakasirikia. Yeye (Subhaanah) ni mjuzi wa kila kitu. Anakiona kila kitu. Lakini kinachokusudiwa ni mtazamo wa hali ya kuridhia na kupenda.
[1] Muslim (2564).
[2] Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Watu aina tatu Allaah hatowatazama siku ya Qiyaamah, hatowatakasa na watakuwa na adhabu kali: mwanaume mwenye kuburuta kikoi chake, mwenye kufanya masimango kwa kile alichokitoa na yule mwenye kuuza bidhaa yake kwa kiapo cha uongo.” Muslim (406).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Fadhwl-il-Islaam, uk. 40
- Imechapishwa: 23/08/2020
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah hatazami miili yenu wala mali zenu; anatazama nyoyo zenu na matendo yenu.”[1]
Nini makusudio ya kutokutazama?
Jibu: Makusudio ya kutokutazama ni kwamba hatilii umuhimu wowote. Hadiyth hii ni kama mfano wa maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Allaah hatowatazama siku ya Qiyaamah na wala hatowatakasa.”[2]
Kwa sababu ya kuwakasirikia. Yeye (Subhaanah) ni mjuzi wa kila kitu. Anakiona kila kitu. Lakini kinachokusudiwa ni mtazamo wa hali ya kuridhia na kupenda.
[1] Muslim (2564).
[2] Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Watu aina tatu Allaah hatowatazama siku ya Qiyaamah, hatowatakasa na watakuwa na adhabu kali: mwanaume mwenye kuburuta kikoi chake, mwenye kufanya masimango kwa kile alichokitoa na yule mwenye kuuza bidhaa yake kwa kiapo cha uongo.” Muslim (406).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Fadhwl-il-Islaam, uk. 40
Imechapishwa: 23/08/2020
https://firqatunnajia.com/anachozingatia-allaah-ni-nyoyo-na-matendo-ya-watu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)