Swali: Vipi ikiwa mtu atauliwa kwa kutetea heshima ya mwanamke wa Kiislamu?
Jibu: Hapana sahaka kuwa ni shahidi kwa sababu amedhulumiwa.
Swali: Hata kama atauliwa?
Jibu: Muuaji ni mwenye kudhulumu na ataingiaMotoni. Dhalimu ni mwenye kukiuka heshima za waislamu. Ni dhalimu. Kunakhofiwa juu yake kuingia Motoni na yuko chini ya utashi wa Allaah.
Swali: Endapo atamuua kwa ajili ya kumtetea yule mwanamke?
Jibu: Muuaji ni mwenye kujitahidi na mwenye kulipwa thawabu. Muuliwaji ambaye alikuwa anajaribu kuyaendea machafu anastahiki kuingia Motoni – kama ilivyopokelewa katika Hadiyth – kutokana na dhuluma yake. Tunamuomba Allaah usalama.
Swali: Vipi ikiwa mshambuliaji huyo anaweza kuzuiwa bila kuuliwa?
Jibu: Anatakiwa kumzuia kwa njia nyepesi zaidi. Njia hiyo ni kama kumpiga na kumtisha kwa maneno. Ikiwa hazuiliki isipokuwa kwa kuuliwa basi atauliwa:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Basi mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
[1] 64:16
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/22934/حكم-من-قتل-وهو-يدافع-عن-عرض-امراة
- Imechapishwa: 18/09/2023
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)