Swali: Vipi ikiwa mtu ataswali nchikavu na asijitahidi kukitafuta Qiblah, alichofanya ni kuanza kuswali wakati tu alipofika.
Jibu: Ikiwa hakufanya juhudi, anapaswa kurudia.
Swali: Lakini alikielekea Qiblah bila ya kufanya juhudi yoyote?
Jibu: Ikiwa alikielekea Qiblah, basi sifa zote njema ni za Allaah.
Swali: Hata kama hakufanya bidii yoyote?
Jibu: Hata kama; muda wa kuwa ameswali akiamini huko ndiko kwenye Qiblah, sifa zote njema ni stahiki ya Allaah. Hilo ndio lengo.
Swali: Hapana, aliswali namna hii tu. Baada ya kuambiwa atafute Qiblah akasema kuwa hapana haja.
Jibu: Maadamu aliswali akiamini huko ndio kwenye Qiblah, sifa zote njema ni za Allaah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/27459/حكم-من-صلى-في-البر-ولم-يجتهد-في-القبلة
- Imechapishwa: 10/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)