Amesimama ´Arafah usiku lakini akakosa kulala Muzdalifah

Swali: Vipi kuhusu mtu aliyesimama ´Arafah usiku kisha akakosa kulala Muzdalifah?

Jibu: Hapana vibaya ikiwa alikuwa na udhuru. Mfano wa hili ni kama hali ya ´Urwah aliyefika Muzdalifah asubuhi ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumwamuru kutoa fidia. Lakini ikiwa mtu alikosa kwa kuzembea, basi anapaswa kutoa fidia.

Swali: Vipi ikiwa mtu atasimama ´Arafah kwa muda wa saa moja tu?

Jibu: Inamtisho ikiwa atawasili mwishoni mwa usiku.

Swali: Nini kipimo cha udhuru kwa mtu aliyekosa kulala Muzdalifah?

Jibu: Kipimo ni ukosefu wa uwezo wa kufika Muzdalifah. Mfano gari lake lilipata hitilafu na hakuweza kufika, amezuiliwa na maradhi, amepotea njia au nyudhuru kama hizo zinazokubalika kwa mujibu wa Shari´ah.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25001/حكم-من-وقف-بعرفة-ليلا-ثم-فاته-المبيت-بمزدلفة
  • Imechapishwa: 23/01/2025