Amekumbuka kuwa hajaswali ´Aswr alipokuwa anaswali Maghrib

Swali: Wakati imamu alipokuwa anaswali Maghrib akakumbuka kuwa hajaswali ´Aswr. Afanye nini katika hali hiyo?

Jibu: Ataendelea kuswali Maghrib. Wakati atakapomaliza kuswali Maghrib, ataswali ´Aswr. Hapo itasihi ´Aswr yake. Haimlazimu kukata swalah yake – na wala haijuzu kwake kufanya hivo. Kwa sababu yule anayeanza faradhi analazimika kuikamilisha isipokuwa kama kuna udhuru unaokubalika katika Shari´ah.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/219)
  • Imechapishwa: 17/04/2026